Mkuu wa 
Jeshi la Polisi Nchini Said Mwema akimkabidhi pikipiki Kamanda wa Polisi
 Kanda Maalumu ya Dar Es Salaam, Naibu Kamishna wa Polisi Suleiman Kova 
kama ishara ya kukabidhiwa Makamanda wote Tanzania bara na Visiwani 
ambapo jumla ya Pikipiki 564 zimekabidhiwa kwa ajili ya kuzuia uhalifu 
kwa lengo la matumizi ya Wakaguzi Tarafa wa Polisi Tanzania bara na 
Majimbo yote ya Zanzibar, program za Safiri Salama na Usalama wetu 
kwanza.
Makabidhiano
 hayo yamefanyika katika makao makuu ya Jeshi la Polisi jijini Dar es 
salaam na kuhudhuriwa na Makamanda na maafisa mbalimbali wa jeshi hilo.
 


 
 
 
 
 
