24Bongo News :
Home » , » TAIFA STARS KAMILI KUIVAA SUPER EAGLES JUMAMOSI

TAIFA STARS KAMILI KUIVAA SUPER EAGLES JUMAMOSI

  • Baada ya maandalizi nchini Uturuki sasa iko kamili kuivaa Nigeria
  • Vicent Enyeama ajitoa Kikosini kwa sababu za kifamilia
  • Mtihani wa kwanza wa Kocha Sunday Oliseh wa Nigeria
  • Taifa Stars haijawahi kuifunga Nigeria
  • Samatta,Mrisho Ngasa na Ulimwengu watabiriwa kuimaliza Nigeria
 Timu ya taifa ya Tanzania,Taifa Stars kesho inaikaribisha timu ya Nigeria katika mechi ya kufuzu kwa fainali za Afrika 2017 kwenye uwanja wa Taifa.Taifa Stars haijwahi kuifunga Nigeria katika mechi za mashindano.

Kikosi cha   Nigeria kinachoundwa na nyota wengi wanaosakata soka la kulipwa nchini Ulaya na kwingineko watakuwa na kazi ngumu ya kuizuia Taifa Stars yenye hali na motisha mpya mbele ya mashabiki.

Stars inayonolewa na Kocha Boniface Mkwasa ilikuwa nchini Uturuki ikiweka kambi kujifua zaidi na kufanya maandalizi ya kutosha kwa ajili ya michuano ya kufuzu.Taifa Stars ilicheza mechi moja ya kirafiki nchinu humu dhidi ya Libya na kupoteza mchezo huo japo timu ilionyesha mabadiliko ya kiuchezaji na kucheza vizuri.


Timu zote mbili zinakutana ikiwa ni baada ya kufanyiko mabadiliko ya ufundi .Upande wa Nigeria ,Kocha Sunday Oliseh ambae amechukua mikoba ya Kocha Stephen Keshi atakuwa ana kibarua kigumu ugenini kuiwezesha timu hiyo inayosukwa upya kuondoka na ushindi huku ikiwa imeshampoteza kipa na mchezai wake mzoefu Vicent Enyeama kwa sababu za kifamilia.Kipa huyo atakuwa ni pengo kubwa kwa Nigeria  hasa ukizingatiwa uzoefu wake kwa mechi za kitaifa.

Huku Taifa Stars ikiwa chini ya benchi jipya la Ufundi likiongozwa na Mkwasa ,ni wazi kwamba ushindi pekee ndo lengo la Taifa Stars kujiweka kwenye mazingira mazuri ya kufuzu fainali za Afrika 2017.Nyota wa kutegemewa wa Stars Mbwana Samatta anaechezea TP Mazembe ataongoza mashambulizi huku akisaidia na Mrisho Ngasa,Thomas Ulimwengu na John Bocco.

Ni matumaini  yetu watanzania tunaondoka na ushindi kwa kuipa nguvu timu yetu ya Taifa Stars kesho.Tukutane UWANJA WA TAIFA.ALL THE BEST TAIFA STARS

Je wewe una maoni gani?!

Share this article :

KIKI POLICY


KIKI BLOG POLICY

Blog hii haina lengo la kumdharirisha mtu na pia kutoa taarifa binafsi zenye lengo la kumkwaza mtu,baadhi ya picha na habari katika blog hii hazimilikiwi na KIKI blog bali zinatoka katika vyanzo mbalimbali vya habari. Ikiwa kuna habari au picha yenye kukudharirisha basi usisite kututaharifu mapema hili iondolewe.
KARIBUNI WOTE

BANK WITH DTB 24/7

Blogger Tips and TricksLatest Tips For BloggersBlogger Tricks

WASOMAJI

Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below

Powered By Blogger Widgets

THIS BLOG IS SPONSORED BY:

THIS BLOG IS SPONSORED BY:

KUMBUKUMBU

ZILIZOVUMA

 
----
Support : Copyright © 2015. KIKI NEWS - All Rights Reserved
This blog Designed by and Modified by Joseph Richard