- Beki wa Uholanzi Bruno Martins alambwa nyekundu mapema
- Glyfi Sigurdsson afunga goli pekee la mchezo huo kwa mkwaju wa penati
- Kwa mara ya kwanza Uholanzi kupoteza mechi ya kufuzu nyumbani
![]() |
Tukio la penati lilozaa goli pekee la mchezo |
Refa aliizawadia Iceland penati yenye utata baada ya beki Van De Wiel kumchezea rafu mchezaji wa Iceland Birkir Bjarnason wakati akijaribu kucheza mpira.Baadae ilionekana wazi Van De Wiel alicheza mpira na haikuwa penati halali.
Glyfi Sigurdsson aliuweka mpira wavuni kwa mkwaju safi wa penati uliomshinda kipa Jasper Cillessen kuipa goli pekee la mchezo huo na kufufua matumaini ya Iceland kufuzu mashindano makubwa katika historia ya nchi hiyo.
Moja ya siku mbaya kwa Uholanzi pale beki Bruno Martins alipotolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kuonekana kumwangusha mchezaji wa Iceland Kolbein Sigthorsson ambao wote kwa pamoja walianguka chini.
Kocha mwa Iceland alisema.."Tunaendelea kwenda juu,haya ni mafanikio makubwa sana kwenye mpira wa miguu kwetu"
Blind nae alisema "Timu ilijipanga vizuri ilicheza kwa umakini na ilikuwa vigumu kupenya ngome yao.Tukio la Bruno ilikuwa ni chanzo cha kupoteza mechi kwani Bruno hakuwa amefanya maamuzi sahihi."