- Welbeck Nje miezi sita
- Giroud mshambuliaji pekee kuingoza timu msimu huu
Arsenal imeeleza kuwa matibabu ya kwenye Goti kwa mchezaji wake Danny Welbeck hayakwenda vizuri na Wiki iliyopita ikaamuliwa afanyiwe operesheni.Welbeck,
aliumia Goti lake mwezi Aprili huku akiwa ameshaifungia timu yake ya Arsenal
mabao 8 katika Mechi zake 34 tangu ahamie hapo kutoka Man United.
Hili ni pigo kubwa kwa Arsenal ambayo haikusajili mshambuliaji kwenye dirisha la usajili la kiangazi lilifungwa jumanne iliyopita.Mfaransa Oliver Giroud anabaki kuwa mshambuliaji pekee wa kutumainiwa katika kikosi hicho.