24Bongo News :
Home » » MASHABIKI WA SOKA ZANZIBAR WAKISHUHUDIA FAINALI

MASHABIKI WA SOKA ZANZIBAR WAKISHUHUDIA FAINALI

Kwa zaidi ya wiki tatu zilizopita, kuanzia tarehe 19 Januari 2013 mpaka 10 Februari 2013 mashabiki wa soka barani Afrika na duniani kote walikuwa hawabanduki katika viti vyao au sofa kwa ajili ya kutizama mashindano makubwa kabisa ya soka barani Afrika ya kuwania Kombe la Mataifa Ya Afrika mashindano ambayo kwa kizungu yanajulikana kama Orange Africa Cup Of Nations.
 
Wenyeji wa mashindano ya mwaka huu walikuwa Afrika Kusini. Jumla ya mechi 32 zilichezwa na zote zilionyeshwa Live bila chenga kupitia channels za SuperSport zinazopatikana kupitia DStv, wakongwe wa digitali.
 
Wakati wa fainali, DStv kupitia kampuni mama ya MultiChoice Tanzania walijumuika na mashabiki wa soka na wadau mbalimbali visiwani Zanzibar katika viota vya Gymkhana Club na Mtoni Marine. Huko palikuwa na special screening ya mchezo huo wa fainali ambapo Nigeria waliibuka mabingwa (kwa mara ya tatu sasa) baada ya kuwalaza Burkina Faso kwa goli 1-0.
 
Kwa mapana na marefu umekuwa msimu wa kufurahi na marafiki na pia kutizama jinsi ambavyo kabumbu linazidi kutamba kama mchezo unaopendwa zaidi sio tu Afrika bali duniani kote.

Je wewe una maoni gani?!

Share this article :

0 comments:

KIKI POLICY


KIKI BLOG POLICY

Blog hii haina lengo la kumdharirisha mtu na pia kutoa taarifa binafsi zenye lengo la kumkwaza mtu,baadhi ya picha na habari katika blog hii hazimilikiwi na KIKI blog bali zinatoka katika vyanzo mbalimbali vya habari. Ikiwa kuna habari au picha yenye kukudharirisha basi usisite kututaharifu mapema hili iondolewe.
KARIBUNI WOTE

BANK WITH DTB 24/7

Blogger Tips and TricksLatest Tips For BloggersBlogger Tricks

WASOMAJI

Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below

Powered By Blogger Widgets

THIS BLOG IS SPONSORED BY:

THIS BLOG IS SPONSORED BY:

KUMBUKUMBU

ZILIZOVUMA

 
----
Support : Copyright © 2015. KIKI NEWS - All Rights Reserved
This blog Designed by and Modified by Joseph Richard