Kwa zaidi ya wiki tatu zilizopita, kuanzia tarehe 19 Januari 2013
mpaka 10 Februari 2013 mashabiki wa soka barani Afrika na duniani kote
walikuwa hawabanduki katika viti vyao au sofa kwa ajili ya kutizama
mashindano makubwa kabisa ya soka barani Afrika ya kuwania Kombe la
Mataifa Ya Afrika mashindano ambayo kwa kizungu yanajulikana kama Orange
Africa Cup Of Nations.
Wenyeji wa mashindano ya mwaka huu walikuwa Afrika Kusini. Jumla ya
mechi 32 zilichezwa na zote zilionyeshwa Live bila chenga kupitia
channels za SuperSport zinazopatikana kupitia DStv, wakongwe wa
digitali.
Wakati wa fainali, DStv kupitia kampuni mama ya MultiChoice Tanzania
walijumuika na mashabiki wa soka na wadau mbalimbali visiwani Zanzibar
katika viota vya Gymkhana Club na Mtoni Marine. Huko palikuwa na special
screening ya mchezo huo wa fainali ambapo Nigeria waliibuka mabingwa
(kwa mara ya tatu sasa) baada ya kuwalaza Burkina Faso kwa goli 1-0.
Kwa mapana na marefu umekuwa msimu wa kufurahi na marafiki na pia
kutizama jinsi ambavyo kabumbu linazidi kutamba kama mchezo unaopendwa
zaidi sio tu Afrika bali duniani kote.
0 comments:
Post a Comment