SIMBA WABANWA TENA LIGI KUU
Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya vodacom simba sc wamebanwa tena na
timu ya jeshi la kujenga taifa (JKT) na safari hii walikuwa ni wakutokea
Oljoro jijini Arusha.Simba sc walikuwa katika uwanja wa shekh Amri
Abeid jijini Arusha kuwakabili JKT Oljoro katika muendelezo wa ligi kuu
ya vodacom.
Simba wakiwa wametoka kutoa sare ya na JKT Ruvu
waliuwanza mchezo vyema kwa kutawala kipindi cha kwanza na katika dakika
ya 6 Mwinyi Kazimoto aliachia shuti la umbali wa mita 30 na kutinga
moja kwa moja nyavuni.Kipindi cha pili hakikuwa kizuri kwa simba
kufuatia Oljoro kulisakama lango la simba na kama wangekuwa makini
wangetoka na ushindi wa goli 3.
Alikuwa Paulo Nongwa katika dakika ya 54 ajipo isawazishia Oljoro na kupelekea mchezo kumalizika kwa sare ya goli 1-1.
0 comments:
Post a Comment