24Bongo News :
Home » » MALI YAITANDIKA GHANA MSHINDI WA TATU

MALI YAITANDIKA GHANA MSHINDI WA TATU

TIMU ya taifa ya Mali jana imeifunga mabao Ghana 3-1 na kumaliza katika nafasi ya tatu kwenye Kombe la Mataifa ya Afrika, wakiipiku Black Stars kwa mwaka wa pili mfululizo kwenye mashindano haya. 

Mshambuliaji Mahamadou Samassa alifunga bao la kwanza kwa kichwa dakika ya 21, Nahodha Seydou Keita akafunga la pili dakika ya 48 na Sigamary Diarra akahitimisha karamu hiyo ya mabao.

  Kwadwo Asamoah aliifungia Ghana bao la kufutia machozi dakika ya 82. Mshambuliaji wa Ghana, Wakaso Mubarak alikosa penalti mapema kipindi cha pili. 

 

Mwaka jana, Mali iliifunga Ghana 2-0 katika mechi ya kuwania nafasi ya tatu. Waliingia kwenye michuano ya mwaka huu wachezaji wakisema wamedhamiria kufanya vizuri ili kuwapa faraja mashabiki wao kwa vurugu za kisiasa zinazoendelea nyumbani kwao. 

Kipigo cha jana ni pigo lingine kwa Ghana, baada ya kuingia Nusu Fainali kwa mara ya nne mfululizo bila kuingia Fainali.

 Ghana iliingia kuwania nafasi ya tatu baada ya kutolewa na Burkina Faso kwa mikwaju ya penalti kwenye Nusu Fainali. Black Stars walitwaa taji la mwisho la Mataifa ya Afrika mwaka 1982.

 

 Kikosi cha Mali: 

Soumaila Diakite, Diawara, Salif Coulibaly, Adama Coulibaly, Tamboura, Ousmane Coulibaly, Kalilou Traore, Mahamane Traore, Mahamadou Samassa (Sigamary Diarra 78), Keita, Diabate.

Benchi: Mamadou Samassa, N'Diaye, Wague, Maiga, Sissoko, Idrissa Coulibaly, Cheick Diarra, Yatabare, Sow, Samba Diakite, Yirango.

 Kadi ya njano: Tamboura. 

Wafungaji wa mabao: Mahamadou Samassa 21, Keita 48, Sigamary Diarra 90.

  Kikosi cha Ghana:

 Dauda, Richard Boateng, Vorsah, Boye (Mensah 46), Afful, Wakaso,Awal, Asamoah, Asante, Atsu (Adomah 70), Gyan (Clottey 75).

  Benchi: Agyei, Pantsil, Annan, Agyemang-Badu, Derek Boateng, Rabiu, Akaminko, Boakye, Kwarasey.Kadi za njano: Wakaso, Vorsah, Asante.Mfungaji wa bao: Asamoah dk82. 

Mahudhurio: 6,000  

Refa: Eric Otogo-Castane (Gabon)

 

 


Je wewe una maoni gani?!

Share this article :

0 comments:

KIKI POLICY


KIKI BLOG POLICY

Blog hii haina lengo la kumdharirisha mtu na pia kutoa taarifa binafsi zenye lengo la kumkwaza mtu,baadhi ya picha na habari katika blog hii hazimilikiwi na KIKI blog bali zinatoka katika vyanzo mbalimbali vya habari. Ikiwa kuna habari au picha yenye kukudharirisha basi usisite kututaharifu mapema hili iondolewe.
KARIBUNI WOTE

BANK WITH DTB 24/7

Blogger Tips and TricksLatest Tips For BloggersBlogger Tricks

WASOMAJI

Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below

Powered By Blogger Widgets

THIS BLOG IS SPONSORED BY:

THIS BLOG IS SPONSORED BY:

KUMBUKUMBU

ZILIZOVUMA

 
----
Support : Copyright © 2015. KIKI NEWS - All Rights Reserved
This blog Designed by and Modified by Joseph Richard