24Bongo News :
Home » , » RAIS MASKINI KULIKO WOTE DUNIANI

RAIS MASKINI KULIKO WOTE DUNIANI

WENGI tunaamini kwamba ukishakuwa rais basi umeuvaa utajiri lakini kwake ni tofauti.Jose Alberto Mujica (77), Rais wa sasa wa Uruguay ambaye amevunja rekodi ya kuwa rais maskini zaidi kuwahi kutokea. Aliingia madarakani kwa tiketi ya chama cha Broad Front Machi Mosi, 2010.

 Tofauti na marais wote duniani, Mujica haishi ikulu badala yake anaendesha maisha yake  eneo la mashambani, mbali kabisa na mjini anakojishughulisha na ukulima wa maua na mazao mengine. Kabla ya kuwa rais, Mujica aliwahi kuwa waziri wa mifugo, wanyama na uvuvi tangu 2005 hadi 2008 alipochaguliwa kuwa seneta na baadaye kuwa rais.

 Kwa nini ni Maskini?

Haamini uwepo wa mungu(atheist),huchangia asilimia 90 ya mshahara wake kwa watu fukara,yatima na wafanyabiashara wadogo wadogo wa kima cha chini huku kiasi kinachobaki anakitumia kununua chakula na pembejeo kwa ajili ya kilimo.


Usafiri wake

Mujica anamiliki gari dogo na chakavu maarufu hapo zamani kama Mgongo wa chura,na anamiliki gari moja tu ambalo analitumia katika shughuli za mizunguko yake kwa sababu alitumii mafuta sana na gharama za matengenezo ni kidogo kwani halisumbui mara kwa mara.

Alipotokea

Mujica amezaliwa katika familia ya wahamiaji kutokea Italy ambayo ilijihusisha na ukulima wa zabibu na maua,hivyo Mujica alikulia na kulelewa mashambani mpaka pale alipoanza kujiusisha na siasa kwenye chama cha wapiganaji wa msituni(guerila).Huyu ndie Jose Mujica rais maskini kuliko wote ambae hali nyama na hakuwahi kuishi Ikulu badala yake alikaa huko mashambani nje ya mji akilima maua.Awali kabla hajawa rasi alikuwa waziri wa Mifugo,wanyama na Uvuvi tangu 2005 hadi 2008 kabla ya kuteuliwa kuwa seneta na baadae Rais.


HONGERA JOSE MUJICA

VIONGOZI WA AFRIKA WAJIFUNZE KITU HAPO KULIKO KUJILIMBIKIZIA UTAJIRI.


Je wewe una maoni gani?!

Share this article :

KIKI POLICY


KIKI BLOG POLICY

Blog hii haina lengo la kumdharirisha mtu na pia kutoa taarifa binafsi zenye lengo la kumkwaza mtu,baadhi ya picha na habari katika blog hii hazimilikiwi na KIKI blog bali zinatoka katika vyanzo mbalimbali vya habari. Ikiwa kuna habari au picha yenye kukudharirisha basi usisite kututaharifu mapema hili iondolewe.
KARIBUNI WOTE

BANK WITH DTB 24/7

Blogger Tips and TricksLatest Tips For BloggersBlogger Tricks

WASOMAJI

Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below

Powered By Blogger Widgets

THIS BLOG IS SPONSORED BY:

THIS BLOG IS SPONSORED BY:

KUMBUKUMBU

ZILIZOVUMA

 
----
Support : Copyright © 2015. KIKI NEWS - All Rights Reserved
This blog Designed by and Modified by Joseph Richard