24Bongo News :
Home » » HALI YA MANUMBA YAZIDI KUWA MBAYA

HALI YA MANUMBA YAZIDI KUWA MBAYA




HALI ya afya ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini (DCI), Robert Manumba ambaye hivi sasa anapumua kwa msaada wa mashine, bado inahitaji uangalizi wa karibu wa madaktari na wauguzi.

Mkurugenzi wa Tiba wa Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam, Jaffer Dharsee alithibitisha hayo jana katika taarifa yake iliyoelezea hali ya Manumba anayeendelea kupatiwa matibabu katika hospitali hiyo.

“Uongozi wa hospitali ya Aga Khan unapenda kuujulisha umma, kwamba DCI Manumba bado yuko hospitali anaendelea na matibabu. Hali ya afya yake bado inahitaji uangalizi wa karibu wa madaktari na wauguzi,” alisema.

Katika hatua nyingine, ndugu, jamaa, marafiki na maofisa wa ngazi mbalimbali wa Polisi waliendelea kufika hospitalini hapo kumjulia hali Manumba ambaye amelazwa katika chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU).

DCI Manumba aliugua ghafla na kulazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Januari 14, kabla ya kuhamishiwa Aga Khan kwa ajili ya uchunguzi zaidi na kulazwa ICU.

Je wewe una maoni gani?!

Share this article :

0 comments:

KIKI POLICY


KIKI BLOG POLICY

Blog hii haina lengo la kumdharirisha mtu na pia kutoa taarifa binafsi zenye lengo la kumkwaza mtu,baadhi ya picha na habari katika blog hii hazimilikiwi na KIKI blog bali zinatoka katika vyanzo mbalimbali vya habari. Ikiwa kuna habari au picha yenye kukudharirisha basi usisite kututaharifu mapema hili iondolewe.
KARIBUNI WOTE

BANK WITH DTB 24/7

Blogger Tips and TricksLatest Tips For BloggersBlogger Tricks

WASOMAJI

Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below

Powered By Blogger Widgets

THIS BLOG IS SPONSORED BY:

THIS BLOG IS SPONSORED BY:

KUMBUKUMBU

ZILIZOVUMA

 
----
Support : Copyright © 2015. KIKI NEWS - All Rights Reserved
This blog Designed by and Modified by Joseph Richard